23 Novemba 2025 - 18:56
Jeshi la Israel Ladai Kumuua Kigaidi Kamanda Mwandamizi wa Hezbollah katika Mji wa Beirut

Kwa mujibu wa kituo cha habari cha Aljazeera, jeshi la Israel limedai kuwa limemuua mmoja wa makamanda wakuu wa Hezbollah katika mji wa Beirut.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la AhlulBayt (a.s) -ABNA-,  dakika chache zilizopita mlipuko ulisikika katika eneo la Dahieh, kusini mwa Beirut, kufuatia shambulio lililofanywa na jeshi la Israel dhidi ya lengo lililokuwa katika eneo hilo.

Kulingana na taarifa za jeshi la Israel, shambulio hilo lilifanyika kwa “usahihi wa hali ya juu”.

Jeshi la utawala wa Kizayuni limetangaza kuwa lengo la operesheni hiyo kusini mwa Beirut lilikuwa Abu Ali al-Tabatabai (Haitham Ali Tabatabai) ambaye wanadai kuwa ni mtu wa pili kwa umuhimu ndani ya Hezbollah.

Habari zaidi zitaendelea kutolewa kadri zitakapopatikana.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha